Bw. Joash Ezekiel Nyitambe ni mtaalamu mahiri waTeknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 27 katika Utumishi wa Umma. Kwa sasa ni Mkurugenzi wa Kitengo cha TEHAMA katika Wizara ya Maji, Dodoma, nafasi aliyoishika tangu mwaka 2009. Amehudumu kama Mjumbe wa Kamati ya Uongozi ya Ushirikiano wa Serikali Wazi (OGP) ya Taifa chini ya Ofifisi ya Rais, Ikulu, na amechangia kama mtaalamu katika mipango mingi ya Sera za TEHAMA za Taifa na e-government. Kabla ya kujiunga na Wizara ya Maji, aliwahi kuwa Msimamizi wa TEHAMA katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni na Mratibu wa Mifumo ya Habari ya Usimamizi chini ya Programu Endelevu ya Dar es Salaam. Bw. Nyitambe ana Shahada ya Uzamili ya Sayansi ya Teknolojia ya Habari na Usimamizi kutoka Chuo Kikuu cha Avinashilingam, India (2006), Shahada ya Uzamili ya Jiografia ya Dijitali kutoka ITC Enschede, Uholanzi (1997), Stashahada ya Juu ya Kiufundi ya Teknolojia ya Habari kutoka City & Guilds of London Institute, UK (2004), na Cheti cha Prince Foundation katika Usimamizi wa Mirad