NEW CONNECTION

  • Mteja anatakiwa kuwa na vitu vifuatavyo ili kujisajili:
  • Hati/hati ya Muda (offer) au mkataba wa mauziano wa kisheria.
  • Picha moja ya rangi ‘‘passport size’’.
  • Nakala ya kitambulisho cha Mpiga kura au Mkazi au kitambulisho cha Taifa.
  • Ndani ya siku saba za kazi kuanzia siku aliyofanya maombi ya awali, mteja atapigiwa simu kuja kuchukua makadirio ya gharama za maunganisho.
  • Mteja ataungiwa maji ndani ya siku saba (7) za kazi baada ya kukamilisha kufanya malipo (IRUWASA) Kwa kutumia control number utakayopewa.
  • Mteja akishaunganishiwa maji ataanza kupata bili yake kupitia ujumbe mfupi kwa njia ya simu ya mkononi kwa namba aliyosajili wakati wa kuomba maji.